Lakini Serikali ya Libya inayotambulika na jumuia ya kimataifa imesisitiza kuwa itahitaji kushirikishwa katika kuratibu operesheni za kijeshi dhidi ya wahalifu hao.
Balozi wa Libya ndani ya Umoja wa Mataifa, Ibrahim Dabbashi, amesema Mamlaka za libya hazijaelezwa chochote kuhusu Operesheni hiyo kwenye milki yake.
Dabbash amesema mipango ya EU pekee haiwezi kumaliza tatizo la wahamiaji haramu isipokuwa jamii ya kimataifa inapaswa kuisaidia Serikali halali ya Libya kuweza kudhibiti mipaka yake hali itakayorahisisha kukomesha wimbi la wahamiaji haramu.
No comments:
Post a Comment