Baada ya mapigano makali kwa siku
kadhaa katika mji wa Ramadi nchini Iraq,hatimaye mji huo kwa sasa
unashikiliwa na wapiganaji wa kundi la IS.
Mapema msemaji wa Gavana wa jimbo hilo amesema kuwa wapiganaji hao wanayashikilia baadhi ya majengo mhimu ya serikali katika jimbo hilo.
Hata hivyo umoja wa Mataifa umelaani hatua hiyo ya IS,ambapo pia Waziri Mkuu wa Iraq Haider al-Abadi amesema kuwa kwa sasa wanajipanga kwa kushirikiana na majeshi ya Shia ili kukabiliana na wapiganaji hao.
No comments:
Post a Comment