Pages

Saturday, 2 May 2015

Liverpool yawika Everton yashindwa

Nahodha wa Liverpool Steve Gerrard alifunga bao la ushindi katika dakika za mwisho kwa upande wa Liverpool dhidi ya QPR ili kuweka matumaini ya Liverpool ya kufuzu kwa dimba la kilabu bingwa Ulaya msimu ujao.
Gerrard alifunga kichwa kizuru kufuatia krosi katika dakika ya 87 ikiwa mabao ni 1-1.

Phillipe Coutinho aliipatia Liverpool bao la kwanza kupitia mkwaju mzuri kabla ya Leroy Fer wa QPR kusawazisha.

Awali Gerrard alikosa mkwaju wa Penalti baada ya beki wa liverpool kuchezewa visivyo.
Phillipe Coutinho
Wakati huohuo Christian Benteke alifunga mabao mawili na kuisadia Aston Villa kuicharaza Everton mabao matatu kwa mawili na hivyobasi kupanda hadi nafasi ya 14 katika jedwali la ligi.

Matokeo mengine ni
Leicester 3 - 0 Newcastle
Sunderland 2 - 1 Southampton
Swansea 2 - 0 Stoke
West Ham 1 - 0 Burnley

No comments:

Post a Comment