Rais wa Colombia Juan Manuel Santos
anasema kuwa utawala wa nchi hiyo haujui ni watu wangapi ambao
hawajulikani waliko kufuatia maparomoko makubwa ya ardhi ambayo yamewaua
zaidi ya watu 50.
Maporomoko nchini Colombia yawaua zaidi ya watu 50
Waakazi wa mji wa magharibi wa Salgar wanasema
kuwa nyumba wanakoishi watu maskini zilisombwa na matope pamoja na mawe
kufuatia mvua kubwa iliyonyesha eneo hilo.
Makundi ya uokoaji yanatafuta kwenye vifusi kujaribu iwapo yatapata manusura.
Rais ameitaja hali hiyo kuwa janga la kitaifa na kusema kuwa atazijenga upya nyumba zilizoaharibiwa.
No comments:
Post a Comment