Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani
Papa Francis amewatawaza watawa wawili wa Kipalestina walioishi katika
karne ya 19 wakati wa utawala wa Ottoman kuwa watakatifu.
Misa ya kuwatawaza watawa 2 wapalestina katika ukumbi wa st Peters Basilica huko Vatican
Watawa
hao wawili walioishi miongoni mwa jamii ya wapalestina waarabu ,bi Marie
Alphonsine Ghattas na Mariam Bawardy watakuwa miongoni mwa watakatifu
watakao tawazwa hii leo katika ukumbi wa kanisa kubwa la papa Francis la
St Peter's Square iliyoko Rome.
Rais wa Palestina Mahmoud Abbas ni miongoni mwa mahujaji 2,000
wakristo waliofika katika makao makuu ya kanisa katoliki huko Vatican.
Hatua
hii inatazamwa na wengi kama chambo cha kuwavutia wakristu katika
maeneo ya mashariki ya kati ambapo wakristu wanahujumiwa na jamii.
No comments:
Post a Comment