Tetesi zinasema kuwa huenda kiungo mshambuliaji, Mbrazil Andrey Countinho akaachwa na mabingwa hao licha ya kuwa na kiwango kizuri ili apatikane straika mahiri mwenye uwezo mkubwa na nguvu.
Klabu za Tanzania zimekuwa zikitolewa katika hatua za awali za michuano ya kimataifa kutokana na ukosefu wa uzoefu wa kutosha na kukosekana kwa washambuliaji mahiri.
Timu hizo zimekuwa katika harakati za kusajili wachezaji wazuri ili kujiandaa. Azam, waliokuwa wawakilishi wa Tanzania katika Kombe la Washindi barani Afrika, inasemekana pia wapo katika mbio za kuongeza nguvu kikosi chao, wakijiandaa na kombe la Shirikisho mwakani, baada ya kushinda nafasi ya pili katika ligi kuu iliyoisha hivi karibuni.
No comments:
Post a Comment