Pages

Wednesday, 3 June 2015

TYGA, KYLIE WANASWA KWENYE DUKA LA VITO

Tygal akiwa na mpenzi wake Kylie Jenner.

KAPO inayokuja juu kwa sasa ya Kylie Jenner, 17, na Tygal, 25, wikiendi iliyopita walinaswa wakiwa kwenye duka la vito chanzo cha habari kilidai walikwenda kununua pete ya uchumba, wakali hao walinaswa huko Beverly Hills, Calfornia nchini Marekani.

Wapenzi hao wamekuwa wakijiachia pamoja mitaani mara kwa mara lakini kukutwa kwao katika duka hilo la vito kunaaminisha kuwa wanataka kupiga hatua zaidi katika uhusiano wao.
Licha ya kusemwa sana kuwa anatoka na mtoto mdogo, msanii huyo Hip hop, Tyga ameripotiwa kujiandaa kumfanyia bonge la sapraizi Kylie, Agosti 18, mwaka huu kwani mrembo huyo atakuwa ametimiza miaka 18. Chanzo kilisema Kylie anatamani kuchumbiwa na anapenda kuona anavalishwa pete.

No comments:

Post a Comment