Pages

Monday, 13 July 2015

JIMBO LA BAGAMOYO LAFUKUTA

KATIKA kuelekea Uchanguzi Mkuu mwaka huu unaotarajia kufanyika Oktoba, vijana wengi wamejitokeza kuwania majimbo mbalimbali na katika Jimbo la Bagamoyo ambalo linashikiliwa na Mbunge Shukuru Kawambwa kwa miaka 10 mfululizo, tayari kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mathew Yungwe amejitokeza kuwania kiti hicho.
Mtangaza nia akisiliza kwa makini.
Akiomba ridhaa ya kulitumikia jimbo hilo kwa wananchi wa eneo hilo katika Ukumbi wa Macho Kodo iliyopo wilayani humo, Yungwe amesema iwapo atapata nafasi ya kuwa mbunge, vipaumbele vyake ni katika sekta ya afya, uchumi na mawasiliano, sekta ambazo zimekuwa na misukosuko kwa muda mrefu.
“Nitahakikisha kila Kikundi cha Saccos kinatoa asilimia tano ya faidi yao kwa ajili ya wazee, suala la migogoro ya ardhi inapungua na pia nitaweka misingi na kuboresha Soko la Samaki ili vijana wenzangu wapate ajili ya kudumu kwa kuuza bidhaa hiyo ndani ya nje ya Bagamoyo,” alisema na kutambulisha kauli mbiu yake ni ‘Fikiria Tofauti Kwa Maendeleo Endelevu ya Bagamoyo’.

(Picha na Habari GPL/Deogratius Mongela )

No comments:

Post a Comment