Pages

Monday, 16 November 2015

Wapalestina 2 wauawa na Waisraeli

Maafisa wa afya wa Palestina wanasema wapalestina wawili wameuawa baada ya vikosi vya Israeli kufyatua risasi katika ukingo wa Magharibi.

Wapalestina wengine watatu wamejuriwa. Duru za kijeshi za Israeli zasema wanajeshi wake wamejeruhiwa katika eneo la Qalandia karibu na kambi ya wakimbizi wa kipalestina ya huko Ramallah.

 
Wanajeshi hao wa Israeli walikabiliwa na upinzani walipokuwa wakibomoa nyumba ya mpalestina mmoja anaeshukiwa kumuua mu-Israeli mwezi juni.


Mapigano hayo ndiyo ya hivi punde zaidi kutokea baina ya Waisraeli na Wapalestina.

Hadi kufikia sasa waisraeli 13 wamepoteza maisha yao huku zaidi ya Wapalestina 80 wakipoteza maisha.

No comments:

Post a Comment