Leo ni siku ambayo mashujaa wawili wanakumbukwa TZ.. Kwanza ni hayati Sheikh Abeid Amani Karume ambaye alikuwa Rais wa kwanza wa Z’bar.. mwingine ni muigizaji nyota wa Bongo Movie, Steven Kanumba.
Irene Uwoya ni mmoja wa wasanii ambao wamefanya sana kazi na Marehemu Kanumba, hiki ameshea na sisi kwenye kumbukumbu hii ya Kanumba;
“Kiukweli
nakumbuka mambo mengi sana.. Kwa sababu Steve kwangu mimi alikuwa mtu
muhimu sana amenifundisha vitu vingi sana.. isitoshe Steve nilikuwa
namjua kabla sijaanza kuingia kwenye sanaa nakumbuka vitu vingi kweli..
alikuwa mshkaji wangu sana mpaka nimeingia kwenye sanaa amenionesha njia
vitu vingi tu tumefanya“
“Kinachoniumiza
zaidi kuna mipango tu mingi ambayo tulikuwa tumepanga na yeye kabla
hajafariki.. siku chache kabla hajafariki tulikuwa wote tumekaa
tumekunywa.. tumeongea vitu vingi sana vya maisha na vya maendeleo kwa
ajili ya tasnia.. baada ya kama siku mbili nikasikia hiyo. Tarehe ya leo
inanikumbusha sana marehemu Steve, kiufupi siipendi siku ya leo.“– Irene Uwoya.
No comments:
Post a Comment