Zaidi ya wapanda milima 200 wameokolewa kuzunguka Mlima Everest, ambao umekumbwa na athari za tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 7.8.
Wakaazi wengi wa mji mkuu Kathmandu wamekuwa wakilala katika mahema kwa wale wasio na makazi au wanaohofia kurudi majumbani kutokana na athari zaidi za tetemeko la ardhi zinazoendelea. Maelfu wamelala nje kwa siku ya pili Jumapili, baada ya tetemeko hilo kuipiga Nepal Jumamosi.
Maafisa wamesema idadi ya vifo au majeruhi ikaongezeka wakati huu ambapo vikosi vya waokoaji vimefanikiwa kufika katika ameneo ya milimani magharibi mwa Nepal.
Mtu mmoja ambaye aliokolewa na helikopta kwenda katika mji wa Pokhara, kilomita 200 kutoka Kathmandu, amesema karibu kila nyumba katika kijiji chake chenye nyumba zaidi ya 1,000 kimeharibiwa, Bwana Darvas ameiambia BBC.
No comments:
Post a Comment