Ripoti za mahakama nchini Burkina
Faso zinasema kuwa mwili ambao unakisiwa kuwa wa raisi wa zamani
aliyeuawa Thomas Sankara utafukuliwa hii leo katika jaribio la kutaka
kubainisha ikiwa ni wake.
Bwana Sankara aliuawa wakati wa mapinduzi mwaka 1987. Sankara alichukuwa uongozi baada ya mapinduzi ya mwaka wa 1983.
Sankara alipinduliwa na Blaise Compaore ambaye aliitawala Burkina Faso hadi mwaka uliopita alipolazimishwa kuondoka na maandamano makubwa katika mji mkuu wa wa nchi hiyo Ouagadougou.
No comments:
Post a Comment