| Aisha Ally akiwa hoi hospitali. |
“Siku ya tukio mwanangu alitumwa na mama yake mkubwa kwenda dukani kumnunulia vocha, sasa wakati anarudi nyumbani njiani alikutana na mbwa huyo akamshambulia kwenye mguu wa kushoto, mkono wa kushoto na mdomoni.
“Mwanangu alijitahidi kupambana naye ili kujiokoa lakini mbwa naye alikuwa na nguvu, akamng’ata sehemu hizo.”
“Baadhi ya watu waliokuwepo dukani waliona, wengine walianza kulia baada ya kumtambua mwanangu, wengine walikimbilia eneo la tukio kwa lengo la kumwokoa, mmoja wao alimpiga teke yule mbwa akatokomea kusikojulikana.
“Ndipo yule mtu aliyempiga teke mbwa na watu wengine walimleta mwanangu nyumbani akiwa anavuja damu sehemu alizong’atwa. Niliumia sana! Na bado nikikumbuka naendelea kuumia.”
Mzazi huyo alisema kwamba, kabla ya kumkimbiza hospitali Aisha, alimpaka dawa aina ya spiriti kwa lengo la kumkausha damu.Aliendelea kusema: “Baada ya hapo tulimkimbiza Hospitali ya Muhimbili, tulipokelewa vizuri lakini cha ajabu hata dawa aina ya yuso tuliambiwa tukanunue nje jambo lililotusikitisha sana.
“Shida kubwa ilikuwa ni mtoto wangu atibiwe hivyo jirani yangu aliyenisaidia gari pamoja na kunisindikiza, alikwenda kununua hiyo yuso, akapakwa na kuchomwa sindano moja, akafungwa majeraha kisha tukaambiwa turudi nyumbani na kupangiwa tarehe nyingine ya kurudi.”
No comments:
Post a Comment