Mabingwa wa ligi kuu ya Vodacom
Tanzania Bara 2014- 2015, Yanga wakishangilia ubingwa wao huo mara baada
ya kumalizika kwa mtanange wao dhidi ya Azam FC, uliopigwa kwenye
Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam jana. Mtanange huo ulimalizika kwa
Azam kushinda Bao 2-1.
Mgeni Rasmi katika Mchezo huo,
Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo, Mh. Dkt. Fenella Mukangara
akimkabidhi Nahodha wa Timu ya Yanga, Nadir Haroub cheti cha pongezi
kutoka kwa Rais wa Shirikisho la Soka Duniani, Sepp Blatter kwa kutwaa
ubingwa wa ligi kuu ya Tanzania Bara 2014 - 2015.Kushoto ni Rais wa TFF,
Jamal Malinzi na wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Yanga, Yussuf Manji.
Mgeni Rasmi katika Mchezo huo,
Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo, Mh. Dkt. Fenella Mukangara
akimpongeza Mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa baada ya kuchaguliwa
kuwa Mchezaji bora wa mwezi wa nne.
Wachezaji wa Timu ya Yanga
wakiingia uwanjani tayari kwa kukipiga na timu ya Azam FC katika mchezo
wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara, katika Uwanja wa Taifa jijini Dar
es salaam jana.
Mwali kabla ya kukabidhiwa kwa wenyewe.






No comments:
Post a Comment