Kampuni ya Apple imetangaza kubuni
programu tumizi mpya inayojumuisha maktaba ya kupeperusha muziki moja
kwa moja kwenye internet, programu ya kusikiliza redio kwenye internet
na njia maalum ambayo wasanii wataweza kubadilishana vibao vya miziki
ambayo bado haijachapishwa rasmi.
App hiyo mpya inajumuisha mfumo wa kubashiri na kupendekeza utakaotumia mwelekezo wa binadamu kuchagua pamoja na sheria ya hisabati ya kutegua kitendawili kwa mifumo au algorithms. Kadhalika Apple imefichua kwamba Uingereza ndiyo itakayokuwa nchi ya kwanza kupata huduma ya kulipia ya Apple Pay nje ya Marekani.
App hiyo mpya inalenga kuzipa upinzani Spotify, Tidal na app nyinginezo za muziki.
"Lakini Spotify ina mbinu yenye matangazo ya kibiashara inayotolewa bure kuisadia kutangaza bidhaa zake jambo ambalo Apple haina."
Huduma hii mpya ya Apple inazindua kituo cha radio cha Beats 1, mtangazaji katika kituo hicho ni aliyekuwa DJ wa BBC Zane Lowe miongoni mwa watangazaji wengine mashuhuri.
App hiyo vile vile ina uwezo wa kufanya kazi pamoja na programu tumizi ya Siri inayotoa msaada wa maelekezo kwa sauti na kuwawezesha watumiaji kuiamuru icheze wimbo kutoka sauti ya filamu au mwaka bila kuhitaji kujua jina la wimbo huo.
No comments:
Post a Comment