Pages

Friday, 5 June 2015

Canavaro afagilia uzi mpya wa Stars

NAHODHA wa Taifa Stars, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amefurahishwa na ujio wa jezi mpya za timu hiyo akitamba kuwa zitawahamasisha kufanya vizuri. Cannavaro alitoa kauli hiyo jana wakati wa hafla ya uzinduzi wa jezi mpya za timu ya Taifa ulioenda sambamba na ugawaji vyeti kwa makundi mbalimbali yaliyotoa mchango kwenye maendeleo ya soka hapa nchini.


“Hizi jezi mpya ni nzuri na zinatia hamasa hasa kutokana na kuwa na rangi zote za bendera ya Taifa jambo ambalo linatupa deni kubwa sisi wachezaji kuipigania timu yetu ya Taifa.Sisi kama wachezaji tunaahidi kupambana ili kutowaangusha Watanzania,” alisema Cannavaro.
Kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), jezi ambazo zitatumika kwa ajili ya mechi za ugenini zitakuwa za rangi nyeupe wakati zile za rangi ya bluu zitatumika kwa ajili ya mechi za nyumbani.
Wakati huohuo kikosi cha Stars kinaondoka leo Alhamisi kwenda Ethiopia kuweka kambi ya siku saba kabla ya kuivaa Misri kwenye mechi ya kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon).

No comments:

Post a Comment