MANDLA MANDELA, mjukuu wa kwanza wa aliyekuwa rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, amehukumiwa kwenda jela au kulipa faini ya kwa kumshambulia na kumtishia kwa bastola mwalimu wa shule moja mwaka 2013.
| Mandla Mandela, mjukuu wa kwanza wa aliyekuwa rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela. |
| Mandla akiwa na babu yake Mzee Nelson Mandela. |
Mandla alipigwa faini ya Randi 10,000 (sawa na fedha za Kitanzania kiasi cha shilingi million 1.7), ambapo mpaka sasa ameshalipa Randi 8,000 na kubaki Randi 2,000 (sawa na fedha za kitanzania kiasi cha shilingi 343,000. Endapo ataamua kutokulipa faini iliyobaki, atafungwa jela miaka miwili.
Mandla alijulikana sana mwaka 2013 ambao hakimu mmoja wa mahakama ya Mthatha alimwamuru kurudisha mabaki ya miili ya baba yake na watoto wengine wawili wa Nelson Mandela huko Qunu, ambako ndiyo sehemu yao ya asili.
Mjukuu huyo wa Mandela alikuwa ameihamisha miili hiyo kwenda katika kituo kimoja cha makumbusho bila ya kushauriana na familia yake.
No comments:
Post a Comment