| Barua ya Afrika kusini kwa FIFA |
Chama rasmi cha upinzani nchini Afrika Kusini ,Demokratic Alliance kimesema kuwa kimewataka maafisa wa polisi siku ya jumatatu kuchunguza kuhusika kwa kiongozi wa maandalizi ya kombe la dunia nchini Afrika kusini Danny Jordan na rais wa shirikisho la soka nchini humo Molefi Oliphant kwa madai ya kutoa hongo ili kupewa maandalizi ya kombe hilo.
Mamlaka ya Marekani inayochunguza ufisadi katika shirikisho la soka duniani FIFA inasema kuwa aliyekuwa afisa mkuu wa FIFA Chuck Blazer alikiri kwamba fedha hizo zilikuwa hongo ya maandalizi hayo kufanywa Afrika Kusini.
No comments:
Post a Comment