Pages

Monday, 14 September 2015

Makamanda wa Sudan K. wakutana Ethiopia

Makamanda wa kijeshi kutoka pande mbili zinazopigana nchini Sudan Kusini wanakutana mjini Addis Ababa nchini Ethiopia kujadili njia za kutekeleza makubaliano ya kusitisha vita.
Makamanda wa Sudan.K wakutana Ethiopia

Mkutano huo utazungumzia masuala yakiwemo kuondolewa vikosi kutoka vitani, kubuni maeneo yasiyo chini ya ulinzi wa kijeshi na kuondolewa kwa wanajeshi wa kigeni kutoka nchini humo.

Makubaliano ya amani yaliyotiwa sahihi mwezi uliopita yakiwa na lengo la kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe hayakutekelezwa huku pande zite zikilaumiwa kwa kukiuka makubaliano hayo.

No comments:

Post a Comment