Mmiliki wa Skylight Band Dk Sebastian Ndege(Jembe
ni Jembe) akicheza moja ya nyimbo ya bendi Skylight. Njoo leo Jumamosi
kwenye Show ya Fahari ya Mwafrika itakayofanyika kwenye kiwanja cha
Escape One ambapo Skylight Band ikisindikizwa na Msanii machachari
Barnaba Classic watadondosha moja ya show kali usisubirie kusimuliwa
njoo wewe na yule.
|
Sam Mapenzi pamoja akiimba kwa hisia kali mbele ya mashabiki wa bendi hiyo (hawapo pichani) waliofika kwenye kiota cha Escape One Mikocheni.
|
Ashura Kitenge (kushoto) akiwa na Kasongo Junior wa Skylight band waiimba na kucheza mbele ya mashabiki wao ndani ya kiwanja cha Escape One Mikocheni
|
Sony Masamba akiendelea kutoa burudani huku akisindikizwa na waimbaji wenzake ndani ya kiota cha Escape One siku ya Jumapili iliyopita.
|
| Burudani ikiendelea |
Mwimbaji
wa bendi ya Skylight Natasha akiwapa mashabiki vionjo vya nyimbo za
taratibu na kutoa burudani ya nguvu kwa wapenzi wa bendi hiyo waliofika
siku ya Jumapili ndani ya Kiota Cha Escape One.
|
| Bendi ya waimbaji wakali wa Skylight ikirindimisha baadhi ya nyimbo zao huku wakiendelea kuzirudi nyimbo kali za Bendi hiyo |
Sam Mapenzi akitoa burudani huku akisindikizwa na wanamziki wenzake ambao ni Sony Masamba(kushoto) na Kasongo Junior(kulia).
|
Bendi ya waimbaji wakali wa Skylight ikirindimisha baadhi ya nyimbo zao
|
| Sam Mapenzi pamoja(Kushoto) na Ashura Kitenge wakiimba kwa furaha huku wakikonga nyoyo mashabiki wa Skylight Band waliofika kwenye kiwanja cha Escape One, Mikocheni |
Kushoto Rapa
mkongwe katika muziki wa Live Joniko Flower pamoja na mwenzake Sony
Masamba wakisababisha mashabiki viuno vyao viweze kuzungushwa mithiri ya
feni.
|
| Ilikuwa noma sana siku ya Jumapili iliyopita maana ilikuwa sio ya kupitwa basi mchuke na ndugu, jamaa au rafiki yako leo uje kuona vitu vitamu kutoka kwenye Bendi ya Skylight |
| Wanaume wa shoka wakilisakata rhumba wakati wa kuwafurahisha mashabiki wa bendi ya Skylight |
| Bendi haiwezi kuwepo bila kuwa na hawa jamaa wakali wanaosababisha Bendi ya Skylight kupaa |
Ule muda sasa ulifika wa kusugua maana ilikuwa ni noma sana
|
| Wanaume wa shoka wakilisakata rhumba wakati wa kuwafurahisha mashabiki wa bendi ya Skylight |
| Mashabiki wa Bendi ya Skylight wakiendelea kukata mauno kutokana na muziki mkali wa bendi hiyo jumapili iliyopita. |
No comments:
Post a Comment