Lakini mwanajeshi wa Marekani aliyejeruhiwa kwenye operesheni hiyo amefariki.
Ndiye mwanajeshi wa kwanza kufariki tangu kuanza kwa operesheni ya wanajeshi wa Marekani dhidi ya IS mwaka jana.
Kwenye operesheni hiyo iliyotekelezwa mapema Alhamisi karibu na mji wa Hawija kaskazini mwa Iraq, wapiganaji wa IS walinaswa na wengine kadha kuuawa, Pentagon imesema.
Jumla ya mateka 70 walikombolewa, maafisa wa ulinzi wamesema, wakiwemo Waarabu wa dhehebu la Wasunni, wanajeshi 20 wa Iraq na wanachama wa IS waliokuwa wakizuiliwa baada ya kushukiwa kuwa majasusi.
Hakuna watu wowote wa asili ya Kikurdi waliokombolewa, maafisa wa Pentagon na Wakurdi wamesema.
No comments:
Post a Comment