Chama cha soka cha England FA, kimempa adhabu Meneja wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho kutokana na utovu wa nidhamu.
| Jose Mourinho |
Meneja huyo wa Chelsea alimshambulia kwa maneno mwamuzi Robert Madley aliyechezesha mchezo wao dhidi ya timu ya Southampton, na kuchapwa kwa mabao 3-1
Mourinho alikasirishwa na Refa Madley kutowapa Penati na kudai Waamuzi wanaogopa kutoa uamuzi kwa Timu yake.
Kauli hiyo iliwafanya FA wamfungulie Mashitaka ya Utovu wa Nidhamu wakidai kauli za Mourinho zinalenga kuonyesha Marefa wanapendelea.
No comments:
Post a Comment