Pages

Wednesday, 31 August 2016

Mwanasheria mkuu wa serikali na utafasiri wa sheria wa za Nchi: Maajabu Mengine


zimepita siku mbili Tangia Mwanasheria Mkuu wa serikali atoe tofasiri ya sheria (Katiba) kuhusu uhuru wa Kuandamana. Kwa mujibu wake (AG) alikuwa ana encounter hatua madhubuti inayosubiriwa kwa hamu na wapenda democrasia Nchini chini ya UKAWA kuandamana na kudai haki yao ya kikatiba ikiwa ni pamoja na kupinga unyanyasaji wa kisiasa, viongozi kuwa Miungu watu na Democrasia kutekwa Nyara na wale wanaojiita kuwa hawajaribiwi...

IBARA YA 20 (1) YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TZ inasema hivi:-

Every person has a freedom, to freely and peaceably assemble, associate and cooperate with other persons, and for that purpose, express views publicly and to form and join with associations or organizations formed for purposes of preserving or furthering his beliefs or interests or any other interests.
Tofasiri yangu: Kila mtu ana uhuru, kwa hiari yake na kwa amani kukusanyika,kujiunga na kushirikiana na watu wengine, na kwa ajili hiyo, kutoa maoni hadharani na kuunda na kujiunga na vyama au mashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi au kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi mengineyo. Hivyo CHADEMA or MTU yeyote anao uhuru wa kuandamana na kufanya mikusanyiko ya Amani so long as havunji sheria za Nchi.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali( AG)

aliweza ku quote ibara ya 20 (2) (c) ya katiba ya jamhuri ya Muungano wa TZ inayosema hivi:
Notwithstanding the provisions of subarticles (1) and (4), it shall not be lawful for any political party to be registered which according to its constitution or policy accepts or advocates for the use of the force or violent confrontation as means of attaining its political goals.
Mchanganuo:
kwa kifungu cha sheria alichotumia AG kujenga hoja yake, hakihusiani na UKUTA movement wala chama chochote kutumia haki yake ya kikatiba kuandamana. sana sana alikuwa anazunguka mbuyu kwa kusema uvunjifu wa amani lakini anashindwa kutoa tofasiri ya kisheria yenye mashiko.

Kwa maana nyingine, hii inatupa tofasiri kwamba:

  1. Mwanasheria mkuu wa serikali anatumika kisiasa
  2. Mwanasheria mkuu wa serikali haijui sheria vizuri. na hii inaturejesha kwenye mkutano mkuu wa wanasheria nchini (TLS) huko Arusha. alitoa speech ambayo mpaka leo ni ngumu kuamini.
  3. Kwamba serikali hii imejaa viongozi incompetent kuwahi kutokea katika Nchi hii.