![]() |
| Mwenyekiti wa Chama cha Waendesha Bodaboda Wilaya ya Kinondoni, Almano Mdede (katikati) akisoma taarifa yake kwa wanahabari (hawapo pichani). |
WAKATI Mwenyekiti wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, akitoa tamko lake la
kuahirisha maandamano yaliyokuwa yamepangwa kufanyika nchi nzima chini
ya wito wa Ukuta kesho Septemba Mosi, viongozi wa vyama vya waendesha
Bodaboda Mkoa wa Dar es Salaam, vimeungana naye kwa kusema kuwa kama
maandamano hayo yangelifanyika wao wasingeshiriki.
![]() |
| …Akiendelea kuongea na wanahabari. Nyuma yake ni baadhi ya viongozi kutoka wilaya za Kinondoni, Ilala na Temeke. |
Alisema kuwa isingewezekana mwanachama
yeyote kubeba abiria aliyevalia sare ya chama chochote kwani hatua kali
kwa ambaye angelithubutu zingelichukuliwa na viongozi wao wa wilaya.
Mbowe ameahirisha maandamano hayo kwa
muda wa mwezi mmoja ili kutoa fursa kwa viongozi wa dini kutafuta
muafaka wa majadiliano na serikali.

