Narendra Modi awasili nchini China
Waziri mkuu wa India, Narendra Modi,
amewasili nchini Uchina kwa ziara ya siku tatu, akipania kuboresha
ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili yenye nguvu barani
Asia.Atafanya mazungumzo na rais Xi Jinping, ambapo mjadala wao pia utagusia taharuki ya muda mrefu mipakani mwa mataifa hayo mawili.
 |
| Narendra Modi |
India pia inatarajiwa kuzungumzia mipango mikubwa ambayo China
inawekeza nchini Pakistan, hatua inayotishia taifa jirani ya India.
Bwana
Modi anazuru makavazi maarufu ya Terracotta warriors na pia anatazamiwa
kuzuru hekalu la kibuddha la Dashang nyumbani kwao rais wa China katika
jimbo la Shaanxi.
No comments:
Post a Comment