Pages

Wednesday, 3 June 2015

Donald Ngoma kutua Jangwani?

MSHAMBULIAJI wa kimataifa Zimbabwe anayeichezea FC Platnum ya kwao, Donald Ngoma, anayehusishwa na mipango ya kutua Jangwani, amefungua kinywa chake na kutamka maneno machache tu akisema: “Yanga ni watamu sana. ”Ngoma ambaye anahitajiwa na kocha wa Yanga, Mholanzi Hans Pluijm, ambaye alithubutu kusema Didier Kavumbagu wa nini wakati unaweza kuwa na mtu kama huyu (Ngoma).
Donald Ngoma, Mshambuliaji wa PLatnum Fc ya Zimbabwe 
Itakumbukwa Mwanaspoti pekee lenye uwezo wa kusafiri popote zinapokwenda timu za soka za hapa nchini ndiyo lilifichua harakati za Yanga kuhitaji huduma ya mshambuliaji huyo.
Kufuatia taarifa nyingi Mwanaspoti liliamua kumsaka mshambuliaji huyo na kufanya mazungumzo naye kwa njia ya simu ya mkononi na akaeleza kila kitu kuhusu kinachomchelewesha kutua kwake kwa Mabingwa hao wa Tanzania;
Mwanaspoti: Habari yako Donald Ngoma
Ngoma: Salama. Nazungumza na nani?
Mwanaspoti: Unaongea na mwandishi wa gazeti bora la michezo Tanzania la Mwanaspoti.
Ngoma: Nashukuru, niambie.
Mwanaspoti: Vipi maendeleo yako na hapo ulipo FC Platinum?
Ngoma:Kila kitu kinaendelea vyema tunaendelea na ligi, japo leo (jana Jumapili) tupo mapumziko kidogo.
Mwanaspoti: Ngoma, hapa Tanzania kuna taarifa nyingi juu yako kuhusu kuja huku likoje hili?
Ngoma: Kuna uwezekano wa hilo kama kila kitu kitakwenda sawa.

No comments:

Post a Comment