KLABU ya Mbeya City imeamua kufanya usajili wake kim ya kimya
kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara kwa kuzingatia mapendekezo ya
kocha, Juma Mwambusi. Haitaki kuwa kama Simba na Yanga zinazosajili kwa
mbwembwe.
Tayari Mbeya City imeshawasainisha wachezaji wawili wapya akiwamo beki Haruna Shamte wa JKT Ruvu na mshambuliaji wa Coastal Union, Joseph Mahundi. Hata hivyo usajili wa wachezaji hao umefanywa kwa kushtukiza na msemaji wa timu hiyo, Dismas Teni alilidokeza gazeti hili kuwa wameshapokea mapendekezo ya kocha Mwambusi, lakini wanafanya kazi zao kimya kimya bila makeke ili kuijenga timu imara kwa msimu ujao.
“Nimepigwa stop kuzungumzia usajili, lakini
tunaendelea na yetu kwa ajili ya kuijenga timu kabambe ya msimu ujao kwa
kuzingatia kile ambacho benchi la ufundi limeagiza kifanywe,” alisema.
Kuhusu kuondoka kwa nyota wao, Deus Kaseke na
Peter Mwalyanzi waliojiunga na Yanga na Simba, Teni alisema mashabiki
hawana sababu ya kuwa na hofu kwani Mbeya City ina hazina kubwa ya
wachezaji ambao wataifanya timu hiyo kuzidi kukimbiza Tanzania.
Alikiri Kaseke na Mwalyanzi waligoma kusainia
mikataba mipya na wao hawakuwa na jinsi kwani tayari walishajua wapi
wanapoenda kwani walishatakiwa tangu ulipoisha msimu wao wa kwanza
katika Ligi Kuu walipomaliza katika nafasi ya tatu nyuma ya Azam na
Yanga.
No comments:
Post a Comment