Pages

Friday, 12 June 2015

MAKAMBA: TUEPUKE USHABIKI NA KUCHAFUANA

 
Naibu Waziri wa Habari Sayansi na Teknolojia na Mbunge wa Jimbo la Bumbuli (CCM) Mh. January Makamba akicheza ngoma pamoja na wanachama wa CCM Mkoa wa Njombe waliojitokeza kumdhamini alipokuwa mkoani humo kusaka wadhamini wakati wa kugombea urai kwa tiketi ya chama hicho.


Mh. January Makamba akicheza ngoma pamoja na wanachama wa CCM Mkoa wa Njombe waliojitokeza kumdhamin.



Mh. January Makamba na mkewe wakiwasili katika ofisi za CCM Mkoa wa Njombe  ambapo walipokelewa na wanachama wa CCM aliokuwa na kikundi cha ngoma.

Mh. January Makamba na mkewe wakisalimana na baadhi ya wanachama wa CCM katika ukumbi mdogo wa CCM mkoani Njombe.



Mh. January Makamba akiwaka sahihi katika kitabu cha wageni katika ofisi za CCM Mkoa wa Njombe.



Mh. January Makamba akipokea fomu yenye majina ya wanachama wa CCM wa Njombe waliomdhamini kutoka kwa katibu wa CCM Mkoa wa Njombe, ndugu Mponzi. Idadi ya wanachama waliojitokeza kuweka sahihi ya kumdhamini ni 72.



Mh. January Makamba akizungumza na wanachama wa CCM waliojitokeza katika Ukumbi mdogo wa CCM Mkoa wa njombe.



Katibu wa CCM mkoa wa Njombe akizungumza na wanaCCM wa Njombe kabla ya kumkaribisha Mh. January Makamba kuzungumza na wanachama wa CCM wa Njombe.



Mh. January Makamba akimsikiliza kwa makini Katibu wa CCM Mkoa wa Njombe, Ngugu Mponzi walipofanya mazungumzo mafupi ofisini kwa Katibu huyo mara baada ya kupokea fomu zenye sahihi za wanachama wa CCM waliomdhamini.

 
Na Mwandishi Wetu
Mbunge wa Bumbuli na Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia, Mheshimiwa Januari Makamba amewaomba wanachama wenzake wa CCM walioko Njombe kutochukulia suala la ugombea kwa ushabiki kiasi cha kuzua mtafaruku ndani ya chama, jambo ambalo ni hatari kwa ustawi wake.
Makamba ameyasema hayo alipokuwa akiwashukuru wanachama wenzake waliojitokeza kumdhamini ili kupata ridhaa ya kuteuliwa kuwa mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
"Najua katika kipindi hiki, ambacho wanachama wengi tumejitokeza kuwania nafasi hii kila mtu ametengeneza kundi la wafuasi ambao wengi wanadhani kwamba kuwa kundi la mtu mmoja basi wewe ni adui wa kundi jingine. Hili ni kosa, sote tunania njema na nchi hii, tujenge mazxingira ya kutooneana haya baada ya kupatikana kwa mgombea mmoja kwa kuungana mkono bila kuchafua wengine", alisisitiza Makamba.
Makamba ameonya pia kuhusu kuchafuana kwa watangaza nia, wenyewe kwa wenyewe ambako kutasababisha kazi nyingine kubwa ya kuanza kumsafisha mgombesa atakayesimamishwa na chama muda utakapofika.
Leo mchana Makamba anatarajiwa kupokea wadhamini mkoani Songea na baadae kuelekea Mbeya mjini ambako pia atafanya zoezi hilo.

No comments:

Post a Comment