| Rais wa Ufaransa Francois Hollande |
Ufaransa imesema kuwa imedhamiria
kutokomeza kitu kinachoitwa makundi ya wapiganaji wa Kiislam,hiyo ikiwa
ni kufuatia shambulio la Kigaidi la mwishoni mwa juma.
Hata hivyo amesema kuwa kampeni za kijeshi dhidi ya IS nchini Iraq na Syria zitaongezwa na kuimarishwa zaidi. Kundi la kigaidi la IS limejitangazia kuwa ndilo lililohusika na mashambulizi hayo katika maeneo ya Bar,Hotelini na kwenye kumbi za starehe, ambapo jumla ya watu 129 waliuawa.
Akizungumza katika muungano wa Mabunge Hollande amesisitiza kuwa katiba inapaswa kurekebishwa ili kuwa na namna nzuri wanayoweza kuitumia muda wote kuliko kutegemea hatua za dharula tu. Hatua nyingine za Mapendekezo ya Rais ni ongezeko la Polisi 5000 ndani ya miaka miwili ijayo na kuepuka kupunguza bajeti ya vyombo vya ulinzi.
No comments:
Post a Comment